ajali iliyohusisha magari matatu likiwemo la Ratco hapo jana na
kupelekea watu kumi kufariki dunia likihusisha Basi la Ngorika lenye
namba za Usajili T770 BKW lililokuwa kitoka jijini Dar es Salaam kwenda
Arusha na lile RATCO lililokuwa likitokeaTanga kwenda Dar es Salaam
yakigongana uso kwa huso na kulihusisha gari lingine dogo aina ya Toyota
Pass T 628 CXE na kusababisha vifo vya abiria 10 na majeruhi zaidi ya
35,ajali hiyo ikitokea eneo la Mbweni Mkata, wilayani
Handeni mkoni Tanga huku chanzo cha ajali hiyo ni gari dogo iliyokuwa
likitaka kulipita lori lililokua mbele yake na ndipo ilipogongana uso
kwa uso na basi la Ratco lililokuwa likitokea Tanga kwenda Dar es
salaam.
Taarifa zinaeleza zaidi waliofariki katika ajali hiyo ni kutoka katika gari la Ngorika watu 7 na lile Dogo watu 3 lakini katika Gari la Ratco abiria wamepata majeruhi na wanaendelea kupata matibabu huku wengine wakiruhusiwa...

