Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr. Parseko Kone katikati akizungumza na ujumbe kutoka Wizara
ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo ulipotembelea Mkoa huo kwa lengo la
kutoa elimu kwa vijana ya jinsi ya
kujikomboa kiuchumi .Wa kwanza kutoka kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha
Uhamasishaji na Uwezeshaji Kiuchumi Idara ya Maendeleo ya Vijana Dr. Steven
Kissui .
Maafisa Kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni
na Michezo Idara ya Maendeleo ya Vijana waliosimama wakifundisha jinsi ya
kuandika mchanganuo wa Mradi.Mafunzo hayo yalifanyika katika Halmashauri ya
Manispaa ya Mkoa wa Singida hivi karibuni.
Imeelezwa
kuwa jukumu kubwa la Tume ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya ni
kuratibu mapambano dhidi ya biashara , matumizi , uingizwaji na usafirishaji wa
dawa za kulevya ikiwa ni pamoja na kutoa taaluma kwa jamii pamoja na kutoa
huduma za tiba na ushauri nasaha kwa watumiaji wa dawa za kulevya .
Hayo
yameelezwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dr Omar Dadi Shajak
wakati akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa robo ya tatu kuanzia Januari hadi Machi kwa kamati ya
Kudumu ya Baraza la Wawakilishi ya kusimamia ofisi za viongozi wakuu wa
Serikali kwenye ukumbi wa mikutano Ofisini Makamu wa Kwanza wa Rais migombani .
Dr Shajak amesema katika kupunguza uingizwaji na usafirishaji wa dawa za kulevya
Tume imetowa mafunzo ya sheria ya dawa za kulevya kwa taasisi mbali mbali
zilizomo kwenye mapambano hayo kama vile Polisi , waendesha mashtaka , mahakimu
, watumishi wa viwanja wa ndege , bandari, TRA, ZRB.


No comments:
Post a Comment