soundcloud

SAHAMA HAMAD 18 - Pata taarifa mbalimbali za Kisiasa, Uchumi, Dini pamoja na simulizi mbali mbali za kusikitisha zikiambatana na Makala pamoja na Tahrir za Kusisimua.. Pia tuwasiliane kupitia +255659887692 AHSANTENI...

Monday, 14 March 2016

#KUMEKUCHA BURUNDI.

#WAJITOA.
Umoja wa ulaya ambao ni mfadhili mkuu wa serikali ya Burundi hii leo umetangaza kusimamisha misaada ya moja kwa moja kwa serikali ya nchi hiyo kufuatia kushindwa kutimiza matakwa ya Umoja huo kutokana na rekodi yake katika masuala ya haki za binadamu.

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini alisema katika taarifa yake kuwa suala la  hali ya kisiasa nchini Burundi linaendelea kuwa jambo la msingi kwa umoja huo na kuwa ili mahusiano kati yaserikali ya nchi hiyo na Umoja huo yarejee katika hali ya kawaida serikali ya Burundi itapaswa kuchukua hatua madhubuti za kurekebisha hali  ya sasa.

Mongherini  amesema  serikali ya  Burundi inapaswa kutekeleza hatua ilizokubaliana nazo na Umoja wa Afrika, Jumuiya ya Afrika mashariki na  Umoja wa mataifa  na kuzungumza na upinzani ili kutafuta suluhisho  mwafaka la kisiasa kwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment