soundcloud

SAHAMA HAMAD 18 - Pata taarifa mbalimbali za Kisiasa, Uchumi, Dini pamoja na simulizi mbali mbali za kusikitisha zikiambatana na Makala pamoja na Tahrir za Kusisimua.. Pia tuwasiliane kupitia +255659887692 AHSANTENI...

Thursday, 23 April 2015

Libya:Waasi wanawazuia wahamiaji 400

 
Wahamiaji wanaoelekea Italy 
 
Mkuu wa utawala wa waasi nchini Libya ameiambia BBC kuwa vikosi vyao vinafanya juhudi ziwezekanazo kuzuia wahamiaji haramu kuabiri meli kuelekea Ulaya .
Khalifa Al-Ghwell - ambaye serikali yake ya uokozi yenye makao yake mjini Tripoli haitambuliwi kimataifa anasema walinzi wa Libya wa mwambao wamekuwa wakiwashikilia karibu wahamiaji mia nne - kutoka nchi za Sahara barani Afrika katika kipindi cha siku chache zilizopita .
Bwana Ghwell amesema kuwa wahamiaji elfu 17 walikuwa wanaishi katika kambi ya hifadhi nchini Libya , lakini ni asilimia karibu tano walioweza kuvuka na kuingia Ulaya.